Ticker

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

Air Tanzania na mipango ya Q400; vipi kuhusu CS300?


Air Tanzania imeainisha mipango yake ya uendeshaji kwa ndege zake mpya mbili aina ya Dash 8-400s zinazotegemewa kuwasili katika nusu ya pili ya mwezi ujao.

Gharama zilizolipwa na serikali ya Tanzania kwa ajili ya manunuzi ya ndege hizo, tayari zilishadokezwa mwezi Juni na waziri wa fedha na mipango, Dr Phillip Mpango wakati wa kuwasilisha bungen taarifa juu ya hali ya uchumi nchini Tanzania.

"Serikali itanunua ndege tatu: Bombardier CS300 moja yenye uwezo wa kubeba hadi abiria 150 na Bombardier Q400 mbili zenye uwezo wa kubeba abiria hadi 80 kila moja," alinukuliwa Dkt Mpango.

Hakuna tarehe ya kuwasili kwa C Series, au uthibitisho wowote kwamba itaagizwa lini kwa ajili ya Air Tanzania, uliotolewa.

Kaimu mkurugenzi mkuu Patrick Itule anasema kuwasili kwa Q400 kutaleta mapinduzi makubwa ya upanuzi katika mtandao wa safari unaomilikiwa na shirika hilo ambapo kwa sasa kuna Kigoma, Mtwara na Mwanza ndani ya nchi na kikanda ni Moroni, Comoro.

Kwa mujibu wa Itule, sambamba na ndege pekee ya Air Tanzania inayofanya kazi kwa sasa, Dash 8-300, hizo Q400 mbili zitatumika hatua kwa hatua kuanza kutoa huduma za safari kuelekea: Dodoma; Mwanza; Arusha; Mbeya; Tabora; Mpanda; Kilimanjaro; Zanzibar; Pemba Wawi; na Bukoba.

Hata hivyo, kuimarika tena kwa Air Tanzania pia kutategemea si tu kuweka sawa madeni yake ambayo iliripotiwa yanakadiriwa kufikia shilingi billion 93 sawa na dola za kimarekani milioni 50.8, lakini pia  idadi kubwa ya wafanyakazi wake wanaokadiriwa wafanyakazi 200 wakiitumikia ndege moja. Tayari utawala wa rais John Magufuli umeripotiwa kuteuwa jopo la wataalam watakao pitia na kubuni  mpango unaofaa kulirejesha shirika hilo la  ndege linalochechemea katika ubora wake..

Katika kuonesha nia ya dhati ya kurejesha Air Tanzania katika sifa yake ya zamani, Waziri wa Kazi, Mawasiliano na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amemsimamisha kazi aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Air Tanzania, Johnson Mfinanga, na vile vile Mkurugenzi wa Uendeshaji, Sadick Muze, kwa kuwa walichagua rubani asiye na sifa/viwango sahihi kwenda nchini Canada kwa ajili ya mafunzo ya ndege, Q400, katika kampuni ya Bombardier (Montréal Trudeau).

Nafasi hiyo ya Mkurugenzi Mtendaji imesha tangazwa kuwa wazi kwa kuajiri hali inayoonesha kuwa bwana Mfinanga sasa kaondolewa kabisa.  Bwana Patrick Itule ndiye anaye kaimu nafasi hiyo kwa sasa.

Post a Comment

0 Comments